Zitto kabwe ahojiwa na Polisi kwa Dakika 138
Asubuhi June 08 2016 Kiongozi mkuu wa chama cha ACT Wazalendo na Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe ameitikia
wito kutoka kwa mkuu wa upelelezi kanda maalum ya Dar es salaam. Zitto
amefika kituoni hapo na ametakiwa atoe maelezo kuhusiana na maudhui ya
hotuba ambayo aliitoa June 5 2016.Baada ya kutoka Zitto ameyaeleza
haya……….
>>>’nimesikitika tu
kwamba sasa hivi tumefikia hali ambayo unapoenda kwenye mikutano kama
kiongozi wa siasa unaanza kufikiria useme nini au usiseme nini, hali
ambayo haikuwepo kwa takribani miaka 10 iliyopita tulikuwa huru kabisa
kuweza kueleza mawazo yetu na hatua mbalimbali za kisiasa’.>>’
takribani kila kitu
tulichokizungumza kwenye mkutano kwa hiyo inaonyesha dhahiri kwamba ile
fursa ambayo tumekuwa nayo siku zote ya kisiasa ya kuweza kujieleza na
kueleza mawazo yetu inaminywa sasa, tusubiri jumatano wanasheria
watakuwa wanafahamu kwamba hili jambo litakwenda mahakamani au litakuaje‘:-Zitto Kabwe
Zitto kabwe ahojiwa na Polisi kwa Dakika 138
Reviewed by Unknown
on
05:35:00
Rating: