SHEMEJI WA WEMA ATANGAZA NDOA NA DADA WA DIAMOND
MAPENZI bwana! Baada ya
kuogelea kwa muda mrefu katika penzi la muigizaji Kajala Masanja,
hatimaye shemeji wa aliyekuwa rafiki wa mwigizaji huyo, Wema Sepetu,
Ahmed Hashimu ‘Petit Man’ ametangaza ndoa na dada wa Mbongo Fleva,
Nasibu Abdul ‘Diamond’, Esma Abdul.
Kilidai kuwa, Petit alichukua uamuzi huo
baada ya kushauriwa na Wema kuwa umri unakwenda na vishawishi ni vingi
hivyo ni bora aoe mapema.“Unajua Petit Man anamheshimu sana Wema kwa
hiyo alipomwambia Petit kuwa umri unazidi kwenda na anahitaji kuwa na
familia yake akaukubali ushauri wake,” kilinyetisha chanzo hicho.
“Acha nipumzike na madhira ya dunia maana huko kote nilipopita hakukuwa chaguo langu ila kwa Esma nimekufa nimeoza bado kuzikwa tu yaani mimi ni mfu ninayetembea mbele ya Esma.”
SHEMEJI WA WEMA ATANGAZA NDOA NA DADA WA DIAMOND
Reviewed by CapchaMuzic
on
00:38:00
Rating: