AY AZUA GUMZO, SOMA HAPA TUKIO ALILOFANYA AMBALO HAKUNA MSANII WA BONGO AMEWAHI FANYA

IMG-20140803-WA0011
Kati ya watu wenye bahati unaweza kusema kuna watu wamekuwa nayo toka wanazaliwa, hii ni mpya kabisa, AY akiwa ndio msanii wa kwanza kuitangaza Tanzania kimuziki huko ughaibuni, na ndipo wakafuatia na wasanii wengine kibao ambao hadi hivi sasa wanaendelea kuitangaza vizuri, ukiachia mbali kuwa yeye ndio anayeongoza kufanya colabo za muziki na wasanii wengi sana wa nje za nchi.
Hii hapa ni kali zaidi, AY anaweka historia akiwa kama msani wa kwanza wa Bongo fleva kukanyaga ikulu ya marekani, hii unaweza kusema ni bahati ya kipekee kwa kuwa, kuna hata baadhi ya watu maarufu na wasanii duniani ambao kwao bado ni ndoto kutia mguu ikulu hiyo ya marekani. Akifunguka zaidi kwa yaliomkuta alisema kwanza, kama yeye kwanza alidhani kuwa ni utani alipopokea barua pepe ya mwaliko huo, cha kushangaza zaidi alichotakiwa ni kutovaa suti siku hiyo, inayosemekana kuwa wakati wa siku kama hizo ni marufuku kuvaa suti katika eneo hilo.
White-House-America-Wallpaper
AY ni zaidi ya msanii ambaye anawakilisha Tanzania si kwa muziki wake tu mkali, unaopendwa na watu wa nchi mbali mbali bali zaidi ni balozi wa UNICEF anayetambulika na mataifa mbali mbali, kujituma kwake kikazi ndiko kulikomfikisha msanii huyu kufika level hizo na kuzidi kukanyaga sehemu adimu kama ikulu hiyo ya marekani.


IMG-20140804-WA0000
AY AZUA GUMZO, SOMA HAPA TUKIO ALILOFANYA AMBALO HAKUNA MSANII WA BONGO AMEWAHI FANYA  AY AZUA GUMZO, SOMA HAPA TUKIO ALILOFANYA AMBALO HAKUNA MSANII WA BONGO AMEWAHI FANYA   Reviewed by Unknown on 03:50:00 Rating: 5
Powered by Blogger.